Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 73 2026-02-02

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:-

Je, nini hatma ya Mradi wa TASAF nchini?

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia kukamilika kwa utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini, Serikali inaendelea na maandalizi ya Awamu ya Tatu ya Mpango ili kuimarisha hifadhi ya jamii nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanza kwa Awamu ya Tatu ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kunathibitisha dhamira ya dhati ya Serikali ya kuiendeleza TASAF kama chombo cha kimkakati cha utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya 2023, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na Mipango ya Maendeleo ya Muda Mrefu, wa Kati na Mfupi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika awamu hii mkazo utawekwa zaidi kwenye Kaya kuhitimu, kujitegemea kiuchumi, ajira pamoja na ushirikishwaji wa kaya katika mifumo ya kawaida ya huduma za Serikali. Ahsante.