Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 75 2026-02-02

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. NAPE M. NNAUYE aliuliza:-

Je, Serikali haioni haja ya kuanza upembuzi wa ujenzi wa reli ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Kusini kufuatia maandalizi ya Mradi wa LNG?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TRC imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya ujenzi wa reli ya standard gauge ya Mtwara – Mbamba Bay na matawi yake ya Liganga na Mchuchuma yenye jumla ya kilometa 1,000. Aidha, kwa sasa Serikali inaendelea na utafutaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, ikiwemo kutumia utaratibu wa ubia baina ya sekta ya umma na binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha Kwa upande wa reli kutoka Dar es Salaam hadi Mtwara, Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia Mpango Kabambe wa East African Railway Master Plan imetambua umuhimu wa kipande hiki cha reli kitakachounganisha Bandari ya Dar es Salaam na Bandari ya Mtwara kutokana na umuhimu wake kiuchumi, kijamii na utengamano wa Kikanda. Hata hivyo, kwa sasa reli hiyo bado haijawekwa katika mipango ya Serikali kwa kutumia fedha za Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kufafanua kuwa, kwa sasa Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Reli ya SGR na miradi mbalimbali ya kimkakati nchini; na miradi hiyo iko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji. Miradi hiyo inatekelezwa kwa awamu kutokana na uhitaji wa fedha nyingi kwa wakati mmoja. Hivyo, nitoe rai kwa wawekezaji kutoka sekta binafsi na kampuni za fedha kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya reli ikiwemo reli ya kusini kwa kuanza na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli hiyo.