Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 5 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 82 | 2026-02-02 |
Name
Charles Mhando Njama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Korogwe Mjini
Primary Question
MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:-
Je, lini barabara ya Old Korogwe – Kwamndolwa kilomita 10 itajengwa kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mhando Njama, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Old Korogwe ni sehemu ya barabara ya Mkoa ya Old Korogwe – Kwamndolwa – Magoma – Mashewa – Bombomtoni – Mabokweni yenye urefu wa kilometa 127.69. Mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Old Korogwe – Kwamndolwa yenye urefu wa kilomita 10 upo katika hatua ya manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi. Mara baada ya kumpata Mkandarasi ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved