Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 82 2026-02-02

Name

Charles Mhando Njama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. CHARLES M. NJAMA aliuliza:-

Je, lini barabara ya Old Korogwe – Kwamndolwa kilomita 10 itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mhando Njama, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Old Korogwe ni sehemu ya barabara ya Mkoa ya Old Korogwe – Kwamndolwa – Magoma – Mashewa – Bombomtoni – Mabokweni yenye urefu wa kilometa 127.69. Mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Old Korogwe – Kwamndolwa yenye urefu wa kilomita 10 upo katika hatua ya manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi. Mara baada ya kumpata Mkandarasi ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza. Ahsante.