Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Health and Social Welfare Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 87 2026-02-02

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:-

Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha wanawake wajasiriamali wanashiriki moja kwa moja kwenye utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka mikakati mbalimbali katika kuhakikisha wanawake wajasiriamali wanashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 hususani Nguzo ya Kwanza ya Uchumi Imara, Jumuishi na Shindani na Nguzo ya Pili ya Uwezo wa Watu wa Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati hiyo ni pamoja na: kupunguza mkwamo na kupanua upatikanaji wa mitaji na masoko kwa wanawake ili kuongeza uzalishaji; kubainisha na kutekeleza jitihada zenye lengo la kuwawezesha wanaume na wanawake kutambua na kutumia fursa za kiuchumi; utekelezaji wa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi; na kuwezesha wanawake kiuchumi kwa kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali, teknolojia na viwanda ili biashara zao zikue na kuchangia uchumi wa Taifa.