Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 88 | 2026-02-02 |
Name
Innocent Lugha Bashungwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karagwe
Primary Question
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA Tarafa za Nyabiyonza na Nyakakika kwani kuna umbali mrefu toka Chuo cha VETA Kayanga?
Name
Omari Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa, Mbunge wa Karagwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Wilaya ya Karagwe, Serikali imejenga Chuo cha VETA cha Wilaya kilichopo Kayanga ambacho kina mabweni na kinaendelea kutoa mafunzo. Kwa sasa wanachi wa Tarafa za Nyabiyonza na Nyakakika wanaweza kuendelea kutumia chuo hicho kwa kuwa kinatoa huduma ya malazi katika mabweni yaliyojengwa kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka umbali mrefu.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved