Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Innocent Lugha Bashungwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karagwe
Primary Question
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA Tarafa za Nyabiyonza na Nyakakika kwani kuna umbali mrefu toka Chuo cha VETA Kayanga?
Supplementary Question 1
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshuruku Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri kwa Wanakaragwe, ninaamini ombi langu kutokana na umbali wa tarafa hizi mbili kwenda kwenye Kituo cha VETA Kayanga Mjini, Wizara itaendelea kulifanyia kazi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Chuo cha VETA pale Kayanga Mjini kipo katikati ya mji na hakina uzio. Je, ni lini Serikali itatujengea uzio?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Chuo kina uwezo wa ku-accommodate wasichana 52, lakini hivi sasa chuo kina wasichana 125. Je, Serikali itatujengea lini bweni lenye uwezo wa kuwa-accommodate wasichana wote? Ahsante sana.
Name
Omari Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Bashungwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza kwa kufuatilia mambo yanayohusiana na jimbo lake, lakini Serikali inatambua kwamba, uhitaji wa uzio kwa Vyuo vya VETA ni kwa vyote vile ambavyo vimejengwa vya wilaya. Serikali inafanyia kazi kwa awamu suala hili ambapo Chuo cha VETA cha Kayanga ni miongoni mwa vyuo ambavyo vipo katika mpango huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili; ninakubaliana na yeye kwamba, bweni lile ambalo lipo sasa hivi la wasichana halitoshi, lakini hatua za dharura zimechukuliwa. Kuna jengo moja la Chuo cha Kayanga limefanyiwa ukarabati, kwa ajili ya kuwaweka wasichana wetu na ujenzi umeshakamilika. Fedha ya kupeleka furniture imetengwa kwa hiyo, muda wowote furniture zitapelekwa na watoto wataanza kutumia bweni hilo ambalo litakuwa na uwezo wa kuchukua wasichana 80.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia imeweka mpango wa muda mrefu wa kujenga jengo la wasichana ambalo litakuwa na uwezo wa kuchukua wasichana 200. Kwa hiyo, naamini wasichana wa Wilaya ya Karagwe watakuwa wapo salama na watapata mafunzo ipasavyo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved