Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 138 | 2026-02-06 |
Name
Hamoud Abuu Jumaa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibaha Vijijini
Primary Question
MHE. SUBIRA K. MGALU K.n.y. MHE. HAMOUD A. JUMAA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha hadhi Mji Mdogo wa Mlandizi kuwa Mji kamili?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamoud Abuu Jumaa ambalo leo limewasilishwa na Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu na nimpongeze kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Halmashauri huanzishwa au kupandishwa hadhi kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa, Sura ya 287 na 288 pamoja na mwongozo wa uanzishwaji wa maeneo ya utawala ambao tumeutoa mwaka 2014, ambao umeainisha vigezo na taratibu zinazopaswa kufuatwa ili kuanzisha au kupandisha hadhi Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa mwongozo mchakato wa kuanzisha Halmashauri mpya huanza na kusudio ambalo hupaswa kujadiliwa katika vikao vya ngazi ya Vijiji/Mitaa, Kata, Halmashauri, Wilaya na Mikoa. Kusudio hilo huwasilishwa Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI kupitia Katibu Tawala wa Mkoa husika kwa ajili ya kufanyiwa tathmini na ufuatiliaji ili kuhakikisha ufikiwaji wa vigezo husika.
Mheshimiwa Spika, ninapenda kuielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kufanya michakato iliyoainishwa kwenye sheria zetu na mwongozo wa uanzishwaji wa maeneo ya utawala.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved