Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 140 2026-02-06

Name

Neema Peter Majule

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. NEEMA P. MAJULE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Mfumo madhubuti wa kupima matokeo ya mikopo 10% ya Halmashauri ili kubaini changamoto na mafanikio?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Dkt. Neema Peter Majule, Mbunge wa Mkoa mzima wa Dodoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kanuni za 31, 32 na 36 za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu za Mwaka 2024 zinaelekeza na kuweka utaratibu wa kufanyika kwa tathmini ya utoaji na usimamizi wa mikopo kila mwaka katika ngazi ya Halmashauri Mkoa na Taifa. Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI imekwishafanya tathmini mara moja tangu kuanza kwa mfumo mpya wa utoaji mikopo. Pia tathmini imekuwa ikifanyika kulingana na changamoto ambazo zinajitokeza wakati wa utekelezaji. Tathmini hizi ndizo zinazowezesha kufanya maboresho mbalimbali mifumo inayotumika.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Januari, 2026, jumla ya vikundi 24,064 vimepata mikopo, ambapo vikundi vya wanawake ni 13,639, vijana ni 8,140 na watu wenye ulemavu ni 2,285. Serikali pia imejenga uwezo kwa wasimamizi 736 wa Halmashauri na 78 wa Mikoa kuhusu usimamizi wa Mfumo wa WEZESHA na inaendelea kuufanyia maboresho Mfumo wa Wezesha ili kuongeza ufanisi na tija ya mikopo kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.