Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 141 2026-02-06

Name

Zuberi Yahya Mfaume

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:-

Je, lini Serikali itadhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji katika maeneo ya Mvuha, Selembala, Dutumi, Kisaki, Bwakila Juu, na Kolelo?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Yahya Mfaume, Mbunge wa Morogoro Kusini:-

Mheshimiwa Spika, kipindi cha kiangazi hutokea adha ya upungufu wa malisho maeneo mengi, ambapo hupelekea wafugaji kuanza kuhama kwa ajili ya kutafuta maji na malisho. Hali hii inasababisha wimbi la wafugaji vamizi kutoka nje ya Wilaya ya Morogoro kuleta mifugo mingi ambayo husababisha mwingiliano na uharibifu wa mazao.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na migogoro, ikiwa ni pamoja na kutenga na kutambua maeneo ya malisho kwa wafugaji kupitia mpango wa matumizi bora ya ardhi, ambapo jumla ya vijiji 68 vimefanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi kwa kutenga hekta 54,577. Watendaji wote wa vijiji na kata kutoruhusu wafugaji wageni kuingia kwenye maeneo yao bila kufuata taratibu, kuhamasisha uzalishaji wa malisho ili kuongeza upatikanaji wa malisho kwa wafugaji.

Mheshimiwa Spika, wizara za kisekta zimeendelea kuimarisha huduma za ugani kwa kutoa elimu ya ufugaji wenye tija wa kuwa na mifugo michache.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine ya ulinzi na usalama kufanya operesheni maalum ya kuondoa mifugo kwenye maeneo ya mashamba ya wakulima katika Wilaya ya Morogoro. Pia, Serikali inapopata tetesi ya mgogoro kwa wafugaji na wakulima, Viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya hufika kwa wakati na kuhakikisha migogoro inatatuliwa.