Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Yahya Mfaume

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:- Je, lini Serikali itadhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji katika maeneo ya Mvuha, Selembala, Dutumi, Kisaki, Bwakila Juu, na Kolelo?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI Y. MFAUME: Mheshimiwa Spika, ninaomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza kutokea katika swali langu la msingi.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; mpaka hivi sasa ninavyozungumza hapa bado kuna mifugo katika mashamba ya wakulima huko katika Jimbo la Morogoro Kusini. Nini kauli ya Mheshimiwa Naibu Waziri sasa hivi ili iweze kutekelezwa na mifugo hiyo iondolewe katika mashamba ya wakulima?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Wizara ina mpango gani sasa katika Jimbo la Morogoro Kusini kuongeza ujenzi wa majosho, malambo pamoja na kasi ya kuelimisha wafugaji juu ya ufugaji bora wa kisasa? Ahsante.

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Mfaume, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze kwa maswali yanayogusa changamoto hizi za wakulima na wafugaji. Sisi Ofisi ya TAMISEMI tunashirikiana kwa karibu sana na Wizara ya Uvuvi na Mifugo na wameendelea kutoa elimu wenzetu Wizara ya Mifugo na pia wanatoa mbegu za ruzuku kwa ajili ya malisho ili kuondoa migogoro hii kabisa.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tunaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuhakikisha mifugo inaondolewa katika maeneo ya wakulima wetu na baadae nitakaa na Mheshimiwa Mbunge pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Mifugo ili tuweze kuyaangazia maeneo haya na kupata ufumbuzi wa kudumu.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali imeendelea kujenga majosho mengi nchini. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge tuweze kuainisha eneo ambalo hasa amelizungumzia ambalo halijapata majosho mpaka sasa ili tuweze kujenga majosho hayo.

Name

Lucy Simirya Kombani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:- Je, lini Serikali itadhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji katika maeneo ya Mvuha, Selembala, Dutumi, Kisaki, Bwakila Juu, na Kolelo?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY D. S. KOMBANI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa hii migogoro imekuwa ya muda mrefu sana na inaleta madhara makubwa sana kwenye hizi jamii zetu na kwa upande mwingine tukiangalia tuna wataalam ambao wamesomea utatuzi wa migogoro; je, Serikali haioni haja sasa ya kuwatumia wataalam hawa katika kumaliza haya matatizo? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, itakumbukwa kwa kipindi cha mwaka 2023 hadi 2025 hakujaripotiwa migogoro yenye kuleta mapigano katika maeneo mengi nchini. Serikali inamuahidi Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kuwatumia wataalam hawa ili kuweka hali hii ya usalama wa wakulima na wafugaji. Tunaendelea kuhamasisha zile kampeni (kwa mfano, Kampeni ya Tutunzane) ili kuona kabisa wakulima na wafugaji wanavyohitajiana na waweze kuishi katika maeneo kwa usalama na uzalishaji mali uendelee.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:- Je, lini Serikali itadhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji katika maeneo ya Mvuha, Selembala, Dutumi, Kisaki, Bwakila Juu, na Kolelo?

Supplementary Question 3

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, ndani ya Jimbo langu la Nanyumbu hivi ninavyozungumza kuna mgogoro mkubwa wa wafugaji na wakulima na kusababisha mashamba ya wakulima kuliwa na mifugo ya wafugaji. Je, Serikali ina kauli gani kuwalazimisha hao wafugaji ambao wamesababisha hasara kubwa kwa wakulima waweze kulipa gharama zote za uzalishaji na badala yake kuwaachia Polisi kushughulikia suala hilo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mhata, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunapozungumzia migogoro ya wakulima na wafugaji ni eneo sensitive sana na Serikali huwa haijiweki katika eneo la kupendelea, hivyo niwaelekeze wahusika wote wa halmashauri za vijiji na halmashauri zetu waweze kufuatilia mgogoro huo na waripoti kwa wakati ili tuweze kwenda kutatua tatizo hilo. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunaweza kuonana baadaye ili tuweze kuona namna gani ya kuli-handle hili bila kuleta pressure katika pande zote. (Makofi)