Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 9 | Energy and Minerals | Wizara ya Madini | 145 | 2026-02-06 |
Name
Chacha Mwita Wambura
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita Mjini
Primary Question
MHE. CHACHA M. WAMBURA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Kituo cha Kuongeza Thamani na Soko la Bidhaa za Dhahabu katika Mji wa Geita?
Name
Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Longido
Answer
NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti kuimarisha uongezaji thamani wa madini katika Mkoa wa Geita ili kuhakikisha manufaa ya rasilimali madini yanabaki nchini. Kutokana na uzalishaji mkubwa wa dhahabu, mkoa huu umewekewa miundombinu muhimu ikiwemo kiwanda kikubwa cha Kusafisha Dhahabu vya Geita Gold Refinery (GGR) na African Eyes Refinery na pia kuna viwanda vidogo vya teknolojia ya kisasa ya uchakataji wa madini ikiwemo mifumo inayojulikana kama (CIP (Carbon in Pulp)/CIL (Carbon in Leach)) pamoja na Vituo vya Umahiri vya Lwangasa na Katente vinavyosimamiwa na STAMICO. Hatua hizi, kwa kuzingatia sheria na sera zilizopo, zimefungua fursa kwa wadau mbalimbali kushiriki katika soko la bidhaa za madini Mjini Geita ikiwepo masuala ya usonara.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kiujuzi, kiuwekezaji na kisheria ili kuimarisha uongezaji thamani madini nchini. Aidha, Wizara kupitia Kituo chetu cha Jimolojia Tanzania (Tanzania Gemological Center) ambacho kiko Arusha) inaendelea kutoa mafunzo ya vitendo ya uongezaji thamani wa madini na kuandaa wataalam wa utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na dhahabu, fedha na vito. Hivyo, nitoe wito kwa Mheshimiwa Mbunge kuwahamasisha vijana wa Mkoa wa Geita hususani Jimbo lake la Geita Mjini kuchangamkia fursa hizi ili kujiajiri, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya Taifa. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved