Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 9 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 146 | 2026-02-06 |
Name
John Francisco Nzilanyingi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyamagana
Primary Question
MHE. JOHN F. NZILANYINGI aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa Uwanja wa Ndege Mwanza utakamilika ili uwe na hadhi ya Kimataifa?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango wa Serikali wa kufanya maboresho makubwa ya Kiwanja cha Ndege cha Mwanza ili kuwa cha kimataifa umeanza. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina unaohusisha ujenzi wa jengo jipya la abiria, upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege, upanuzi wa eneo la maegesho ya ndege na ujenzi wa barabara za kiungio unaendelea.
Mheshimiwa Spika, ujenzi utaanza mara baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved