Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 146 2026-02-06

Name

John Francisco Nzilanyingi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. JOHN F. NZILANYINGI aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Uwanja wa Ndege Mwanza utakamilika ili uwe na hadhi ya Kimataifa?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mpango wa Serikali wa kufanya maboresho makubwa ya Kiwanja cha Ndege cha Mwanza ili kuwa cha kimataifa umeanza. Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina unaohusisha ujenzi wa jengo jipya la abiria, upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege, upanuzi wa eneo la maegesho ya ndege na ujenzi wa barabara za kiungio unaendelea.

Mheshimiwa Spika, ujenzi utaanza mara baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika.