Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 131 2026-04-20

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko kubwa la Mazao ya Kilimo Wilaya ya Mkalama kama ilivyoahidi kwenye Ilani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kujenga soko la mazao katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama. Kwa kutambua umuhimu huo, tayari Halmashauri imepima na kupata hati miliki ya eneo la ujenzi wa soko lenye ukubwa wa ekari 7.2 katika Kata ya Nduguti ambapo ni Makao Makuu ya halmashauri na tathmini ya mazingira katika eneo hilo imefanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi inayoendelea ni kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa mradi huu ambao unatarajia kukamilika Juni, 2026. Baada ya upembuzi yakinifu kukamilika Serikali itatenga bajeti na kuanza ujenzi wa soko hilo. Ahsante.