Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 12 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 133 | 2026-04-20 |
Name
Lucy Edward Mwakyembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapa ajira vijana wanaojitolea?
Name
Regina Ndege Qwaray
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Edward Mwakyembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma ya mwaka 2008, Toleo la Pili, ikisomwa pamoja na Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298 na Mwongozo wa Kujitolea katika Utumishi wa Umma wa Mwaka 2025, ajira katika Utumishi wa Umma hupatikana kwa ushindani na uwazi. Kujitolea katika Utumishi wa Umma huwezesha vijana kujipatia ujuzi wa ziada pamoja na kuwapa uzoefu na uwezo wa kushindana pindi ajira zinapotangazwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo vijana wote wanaohitimu vyuo wanapata fursa ya kujitolea katika Taasisi za Serikali hivyo, utaratibu uliopo wa ushindani unatoa fursa sawa kwa vijana wote wanaojitolea na ambao hawajapata fursa ya kujitolea. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved