Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 136 2026-04-20

Name

Haiderali Hussein Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilongero

Primary Question

MHE. YOHANA S. MSITA K.n.y. MHE. HAIDERALI H. GULAMALI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutekeleza ahadi ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA Ilongero?

Name

Wanu Hafidh Ameir

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba kujibu swali Namba 136 la Mheshimiwa Haiderali Hussein Gulamali, Mbunge wa Ilongero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) 65 katika Wilaya Sitini na Nne (64) na Mkoa mmoja (01) wa Songwe. Ujenzi huu unafanyika katika Wilaya au Mkoa ambao hauna Chuo cha VETA kabisa. Jimbo la Ilongero lipo katika Wilaya ya Singida ambapo tayari ina Chuo cha VETA. Hivyo, wananchi wa Jimbo la Ilongero wanahimizwa kutumia Chuo cha VETA Singida ambacho kina huduma za bweni kwa wanafunzi wanaotoka maeneo ya mbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jitihada za kupanua fursa za upatikanaji na elimu ujuzi kwa ngazi mbalimbali, Serikali inaendelea na ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Amali katika Jimbo la Ilongero ambayo itatoa mafunzo ya vitendo na stadi zinazohitajika katika soko la ajira.