Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo 137 2026-04-20

Name

Mariam Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:-

Je, wananchi wa Temeke wananufaikaje na uwepo wa Uwanja wa Taifa uliopo Wilayani humo?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA, NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa Benjamin Mkapa una faida nyingi kwa wananchi wa Manispaa ya Temeke na Taifa kwa ujumla. Kiuchumi unachochea mzunguko wa fedha kwa wafanyabiashara wakati wa matukio makubwa, pia unavutia wawekezaji wa matangazo makubwa na ajira kwa wananchi. Kijamii, matukio makubwa ya kidini na matamasha makubwa ya sanaa na muziki yanawaleta Wanatemeke na Watanzania wote pamoja na hivyo kudumisha amani na mshikamano wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimichezo uwepo wa uwanja huu umeifanya Manispaa ya Temeke kuwa kitovu cha michezo ya kitaifa na kimataifa jambo linaloongeza heshima na utambulisho wa eneo hilo na kutoa hamasa kwa vijana kushiriki michezo. Hivyo, miundombinu hii ni muhimu katika kuchochea maendeleo kwa wananchi wa Temeke na Tanzania kwa ujumla.