Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 139 2026-04-20

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga uzio wa Uwanja wa Ndege Urambo ili kuutunza vema Uwanja huo na kuwa salama?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuimarisha ulinzi na usalama katika Kiwanja cha Ndege cha Urambo na hivyo inakubaliana na pendekezo la ujenzi wa uzio katika kiwanja hicho. Katika hatua za utekelezaji, suala hili tayari limejumuishwa katika rasimu ya Mpango Mkakati wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wa miaka mitano ijayo, ili kuwezesha upangaji na upatikanaji wa rasilimali fedha kupitia bajeti ya maendeleo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya ukarabati, uboreshaji na upanuzi wa viwanja vya ndege nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kupitia TAA inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa Kiwanja cha Ndege cha Urambo kinaendelea kuwa salama. Hatua hizo ni pamoja na utekelezaji wa maelekezo ya kitaifa kuhusu ulinzi na usalama wa viwanja vya ndege, pamoja na kuimarisha ushirikishwaji wa wananchi wanaozunguka eneo la kiwanja kupitia dhana ya ulinzi shirikishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kiwanja hicho kinamiliki hati ya ardhi, jambo linalosaidia kulinda mipaka yake dhidi ya uvamizi na matumizi yasiyoidhinishwa, hususan katika mazingira ambayo kiwango cha shughuli za kiuendeshaji bado ni cha chini. Serikali itaendelea kuchukua hatua stahiki kadri itakavyohitajika ili kuhakikisha usalama na maendeleo endelevu ya miundombinu hiyo muhimu.