Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 140 2026-04-20

Name

John John Nchimbi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. TIMIDA M. FYANDOMO K.n.y. MHE. JOHN J. NCHIMBI aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa mikopo nafuu ya Boti za Uvuvi za Fiber kwa Wavuvi wa Wilaya ya Nyasa?

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, ninaomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa John John Nchimbi, Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani kwa ajili ya kufanya biashara ndogo, za kati na kampuni changa. Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ilitoa tangazo tarehe 4 Machi, 2026 ili kuujulisha umma juu ya fursa ya mikopo nafuu kwa vijana ili kupata mitaji na kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mikopo hiyo inalenga kutoa vifaa na pembejeo muhimu za ufugaji samaki kwa vizimba, zana za uvuvi, ufugaji wa kuku, ufugaji wa nguruwe, ufugaji wa mbuzi na kondoo, miundombinu ya ubaridi, uchakataji wa dagaa pamoja na mwani katika maeno yote ya wavuvi hapa nchini; wakiwemo wavuvi wa Wilaya ya nyasa. Ninatoa rai kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kuwahamasisha vijana kujiunga kwenye vikundi na vyama vya ushirika ili waweze kunufaika na mikopo hii isiyokuwa na riba na yenye masharti nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha