Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 142 2026-04-20

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:-

Je, lini Serikali itarejesha Kiwanda cha Chai cha Wakulima wa Chai Lupembe (MUVYULU)?

Name

Denis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, ninaomba nijibu swali namba 142 kama lilivyoulizwa na Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda cha Lupembe Tea Factory kilichopo wilaya ya Lupembe kilibinafsishwa mwaka 2004 kwa Kampuni ya Dhow Mercantile Limited. Ubinafsishaji huo uliipa kampuni hiyo 70% ya hisa na 30% ya hisa kubaki kwa Chama cha Ushirika cha Wakulima wa Chai (MUVYULU). Baada ya ubinafsishaji, kulizuka mgogoro kati ya pande hizo mbili; hivyo, uendeshaji wa kiwanda na umiliki wa kiwanda uliosababisha DML kufungua kesi mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadaye pande hizo mbili zilikubaliana ya kumaliza mgogoro huo nje ya Mahakama chini ya usimamizi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina; ambapo kikao cha mwisho kilifanyika tarehe 13 Machi, 2026. Maazimio ya kikao hicho yanaendelea kufanyiwa kazi, ambapo ikikamilika, zoezi la kurejesha kiwanda litafanyika.