Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Je, lini Serikali itarejesha Kiwanda cha Chai cha Wakulima wa Chai Lupembe (MUVYULU)?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza niishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza, wananchi wa Lupembe wanasubiri kwa hamu sana kiwanda hiki cha chai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa Mahakama Kuu ilitoa amri kiwanda kirejeshwe kwa wananchi tangu mwaka 2022, lakini pia Mheshimiwa Rais kwa kuwapenda wananchi wa Lupembe na ili kuwapelekea tabasamu wananchi hawa alikwishaelekeza kiwanda hiki kirejeshwe kwa wananchi tangu 2022 akiwa pale Mtwango. Je, ni nani anayechelewesha huu mchakato mpaka leo kiwanda hakijarudi kwa wananchi wa Lupembe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; wananchi wangu wa Tarafa ya Lupembe kwa maana ya Kata za Idamba, Filiga, Lupembe, Matengwe, Ukalawa pamoja na Kidegembye na Lupembe yenyewe wanalima sana chai kwenye mvua nyingi, wanakaa kwenye mabanda kwa muda mrefu, lakini bei ya chai ni 360 ambayo ni ndogo sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza bei ya chai hadi shilingi 1,000 kwa kilo?

Name

Denis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mbunge Edwin Swalle kwa kupigania sana zao la chai humu Bungeni. Ninaomba nikubaliane naye kwamba kuna maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba, kiwanda hiki kinarudi kwa wakulima kwa ajili ya kuendelea na shughuli za uzalishaji ili kuongeza thamani ya zao la chai, zao ambalo ni la kimkakati kwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TIRDO ambayo ni taasisi chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, ilishaanza zoezi hilo la tathmini mwaka 2024 ikikamilisha tathmini ya majengo na mitambo, changamoto ambayo walikumbana nayo ilikuwa ni kufanya tathmini ya ardhi. Chama cha Ushirika cha MUVYULU ilitakiwa kutoa hati hiyo ambayo kwa kuchelewesha kwao kulipelekea TIRDO kukwama na zoezi la kukamalisha zoezi la tathmini la kiwanda hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kikao ambacho kilifanyika tarehe 13 Machi, 2026 chini wa Wizara ya Kilimo ambacho kilihusisha Ofisi ya Msajili wa Hazina, Wizara ya Viwanda na Biashara, Bodi ya Chai, Mamlaka ya Wilaya kule Njombe, Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Chama cha Ushirika chenyewe pamoja na mwekezaji, walikubaliana kwamba Chama cha Ushirika kiwasilishe hati hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninafarijika kulitaarifu Bunge lako kwamba hati hiyo imeshawasilishwa tayari, wakati utawala wa mkoa na tayari ameshawasilisha kwa Bodi ya Chai. Hivyo, maelekezo yetu ni TIRDO kurudi kwa ajili ya kukamilisha tathmini hiyo ili Hazina wakamilishe malipo kwa mwekezaji, kiwanda hicho kirudi kwa wakulima na kuendelea na uzalishaji na ongezeko la thamani ya zao la chai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.