Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 12 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 143 2026-04-20

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Kasindaga – Kyebitembe – Karambi hadi Runazi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Kasindaga hadi Runazi yenye urefu wa kilometa 37.6 ni barabara ya mkoa, inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Kagera. Kwa sasa, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi.