Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 372 2026-05-19

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga zahanati Kijiji cha Zugumlole itakayohudumia Vitongoji vya Kaung’ando, Ibasa “A” na “B”, Mkombozi, Ulinda na Ndevelwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Zugumlole kipo katika Kata ya Ndevelwa, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora. Kijiji hicho kina jumla ya wakazi 1,989, kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022. Kwa sasa wananchi wa Kijiji cha Zugumlole wanapata huduma katika Zahanati ya Ndevelwa iliyopo kilometa 25 kutoka kijijini hapo. Aidha, kwa upande wa huduma za upasuaji wanahudumiwa kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora iliyopo kilometa 42.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka na umuhimu wa kuwepo kwa zahanati katika Kijiji cha Zugumlole, Serikali ya Wilaya ya Tabora ilifika na kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Zugumlole na kuhamasisha wananchi ili waanze ujenzi wa boma la zahanati na Serikali itatoa fedha za kukamilisha boma kadri utaratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi kote nchini kwa awamu. Ahsante.