Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 374 2026-05-19

Name

Dickson Nathan Lutevele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DICKSON N. LUTEVELE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga stand ya kisasa ya mabasi Halmashauri ya Mji wa Mafinga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dickson Nathan Lutevele Villa, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mapango wa kujenga stand ya kisasa ya mabasi katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga katika Kata ya Kinyanambo kupitia Mradi wa Kuboresha Miundombinu ya Miji (TACTIC) Awamu ya Tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upembuzi yakinifu na usanifu wa awali ulikamilika mwezi Februari, 2026 na taarifa ilishawasilishwa kwa timu ya uratibu wa miradi ya Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI na Halmashauri ya Mji wa Mafinga. Kwa sasa Mtaalam Mshauri Kampuni ya Botek Bosphorus Consulting Corporation kwa kushirikiana na kampuni ya Building design Authority (P) Ltd wanaendelea kufanya usanifu wa mwisho ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2026.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya usanifu kukamilika, hatua itakayofuata ni kutangaza zabuni kwa ajili ya kupata mkandarasi mjenzi. Pindi taratibu hizo zikikamilika, ujenzi wa stand ya mabasi katika mji wa Mafinga utaanza mara moja. Ahsante.