Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dickson Nathan Lutevele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DICKSON N. LUTEVELE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga stand ya kisasa ya mabasi Halmashauri ya Mji wa Mafinga?

Supplementary Question 1

MHE. DICKSON N. LUTEVELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza, naishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini nilikuwa na swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na utaratibu baada ya upembuzi yakinifu kufanyika, kuchelewesha sana mkandarasi kuanza kazi. Stand hii, sisi Halmashauri ya Mji wa Mafinga mpaka sasa hatuna stand. Pale ambapo mabasi yanasimama ni kandokando ya barabara, eneo ambalo limekuwa na ajali nyingi sana, lakini kwa sisi Wana-Mafinga pia, stand hii tunaisubiri kama moja kati ya vyanzo vya mapato kwa sababu mji wetu una msongamano mkubwa sana wa magari, lakini hatuna stand.

Je, nini kauli ya Serikali, ni kwa uharaka upi kwenye kuhakikisha kwamba stand hii, pindi tu upembuzi utakapokuwa umekamilika, tunapata mkandarasi na stand hii inajengwa kwa sababu Wana-Mafinga wameisubiri stand hii kwa muda mrefu sana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza, nimpongeze sana Mheshimiwa Dickson Nathan Lutevele, Mbunge wa Mafinga Mjini, amefuatilia mara kadhaa kuhakikisha kwamba ujenzi wa stand ya kisasa ya mabasi ya mji wa Mafinga inafanyika. Nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini kwamba ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba stand hiyo inajengwa mapema iwezekanavyo na ndiyo maana tayari tumeshafanya hatua za awali za usanifu na upembuzi yakinifu na tuko hatua ya pili ya mtaalamu mshauri ambaye anakamilisha kazi yake mwezi Mei mwaka huu, kwa maana ya mwezi huu mwishoni. Tutahakikisha baada ya ukamilishaji huo, tunaendelea na taratibu zetu za Serikali pamoja na Benki ya Dunia ili kutoa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi huo.

Kwa hiyo, kauli ya Serikali Mheshimiwa Mbunge ni kwamba dhamira yetu ni kuhakikisha tunaanza ujenzi mapema iwezekanavyo baada ya hatua hizi kukamilika.