Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 375 2026-05-19

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuondoa mgongano wa Vikao vya Bunge na Halmashauri za Majiji, Manispaa na Miji ili Wabunge washiriki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwenye nyakati tofauti, imekuwa ikitoa maelekezo kwa halmashauri ili kuhakikisha kwa kiwango kikubwa, ratiba za vikao vya halmashauri hazigongani na ratiba za Vikao vya Bunge. Halmashauri zilielekezwa kuzingatia kalenda ya shughuli za Bunge wakati wa kuandaa kalenda zao za vikao vya mwaka husika ili kutoa fursa kwa Wabunge ambao ni wajumbe wa mikutano hiyo, kushiriki kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, itaendelea kuzisimamia halmashauri kuhakikisha zinaandaa ratiba ya vikao kwa mwaka 2026/2027 kwa kuzingatia ratiba za vikao vya Bunge kwa kadri itakavyowezekana. Aidha, Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini, wanaelekezwa kuwasiliana na Waheshimiwa Wabunge wakati wa kupanga ratiba za Vikao vya Kamati na Mabaraza ya Madiwani, ili kuona namna viongozi hao wanaweza kushiriki katika vikao hivyo. Ahsante.