Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 377 2026-05-19

Name

Kassimu Amari Mbaraka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. KASSIMU A. MBARAKA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Bandari ya Tanga - Kilimanjaro - Arusha - Singida hadi Musoma (kilometa 1108) utaanza?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassimu Amari Mbaraka, Mbunge wa Tanga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TRC imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya kuunganisha reli ya Bandari ya Tanga na Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Singida hadi Musoma. Kwa sasa hatua inayoendelea ni kuhuisha yaani review tafiti hizo, ili kuendana na mahitaji ya sasa ikiwemo ushirikishwaji wa makampuni ya madini yanayowekeza kwenye ushoroba huo. Aidha, Serikali inaendelea na kufanya majadiliano na kampuni mbalimbali ili kufanya uwekezaji wa reli hii ya kimkakati.