Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 377 | 2026-05-19 |
Name
Kassimu Amari Mbaraka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tanga Mjini
Primary Question
MHE. KASSIMU A. MBARAKA aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Bandari ya Tanga - Kilimanjaro - Arusha - Singida hadi Musoma (kilometa 1108) utaanza?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassimu Amari Mbaraka, Mbunge wa Tanga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TRC imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya kuunganisha reli ya Bandari ya Tanga na Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Singida hadi Musoma. Kwa sasa hatua inayoendelea ni kuhuisha yaani review tafiti hizo, ili kuendana na mahitaji ya sasa ikiwemo ushirikishwaji wa makampuni ya madini yanayowekeza kwenye ushoroba huo. Aidha, Serikali inaendelea na kufanya majadiliano na kampuni mbalimbali ili kufanya uwekezaji wa reli hii ya kimkakati.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved