Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Kassimu Amari Mbaraka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tanga Mjini
Primary Question
MHE. KASSIMU A. MBARAKA aliuliza:- Je, lini ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Bandari ya Tanga - Kilimanjaro - Arusha - Singida hadi Musoma (kilometa 1108) utaanza?
Supplementary Question 1
MHE. KASSIMU A. MBARAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa hii ndiyo reli ya kwanza kujengwa, ndani ya Taifa hili la Tanzania wakati huo ikiitwa Tanganyika. Je, Serikali ina mpango gani sasa kuimarisha na kuiboresha reli ya meter gauge yaani MGR, kuweza kutoa shehena nyingi, kubwa na kutosha kutoka pale Tanga, Kilimanjaro hadi Arusha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza, je, ni upi mpango wa Serikali kukifanya sasa Kituo cha Pugu, Pugu Station kwenye reli yetu ya mwendokasi inayoenda speed ili ya express, kuweza kukifanya kuwa sasa ni kituo kama kituo kingine cha kushukia, tuseme cha tatu kutokea Dodoma na pia kutokea Dar es Salaam kiweze kutumika effectively, kwa reli ya mwendokasi inayoenda speed. Ni lini Serikali itakifanya kile kituo ni cha muhimu? (Makofi)
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Kassimu Amari Mbaraka kwa maswali yake ya nyongeza na nampongeza jinsi anavyofuatia maendeleo ya Mkoa wa Tanga na Kaskazini kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Serikali inasimamia Reli ya meter gauge yenye urefu wa kilometa 2,707 ambayo ilipokuwa inajengwa ufanisi wake ilikuwa ni kubeba mzigo wa takribani tani milioni tano. Kutokana na changamoto mbalimbali, reli ya Kati pamoja na Kaskazini uwezo umeshuka mpaka umefika takribani 290,000 sawa na 5.8%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari maboresho yameshaanza kwa upande wa reli ya kati na tayari ninavyozungumza Serikali imeshaagiza material kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapata vitendea kazi vya kuanza ujenzi wa kutoka Ruvu kuelekea Dar es Salaam na hatua ya pili itakuwa kutoka Ruvu - Tanga mpaka Kilimanjaro, ili kuhakikisha kwamba tunaijengea uwezo kutoka kwenye speed ya ratili 20 mpaka 15 iliyopo sasa iweze kwenye uwezo wake wa 80 mpaka 70.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yake ya pili kuhusu Kituo cha Pugu ili tuweze kuongeza. Msingi wa reli ya kisasa ni kufupisha safari. Tunayo treni yetu ya kawaida inayofanya safari zake za kawaida kutoka Dar es Salaam mpaka Dodoma, na kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro na Morogoro mpaka Dar es Salaam na kadhalika ambayo kutoka Dar es Salaam mpaka hapa tuna vituo karibu 10. Serikali iliamua kuweka treni nyingine ya express ambayo inatoka Dar es Salaam mpaka Morogoro, ikitoka Morogoro kituo kinachofuatia ni hapa. Tumepokea maombi yake, lakini msingi tulidhani kwamba, tuendeleze ratiba hii kwanza, ikionekana kuna uhitaji sana baada ya uchambuzi wa kina tutafanya hivyo, kwa muda huu tunawashauri abiria wa pale Ruvu waweze kupanda treni ya kawaida ya kisasa ambayo na yenyewe inatumia masaa kama manne tu, na hii nyingine ni kama karibu masaa matatu na robo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved