Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 378 2026-05-19

Name

John Francisco Nzilanyingi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. JOHN F. NZILANYINGI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya njia nne kutoka Mjini – Usagara na kutoka Mjini – Kisesa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa John Francisco Nzilanyingi, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha usanifu wa kina wa barabara za kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara na kutoka Mwanza Mjini hadi Kisesa kwa ajili ya ujenzi wa njia nne kwa kiwango cha lami. Ujenzi wa barabara hizi utafanyika kwa awamu ambapo kwa sasa Serikali iko katika hatua ya mwisho ya manunuzi ya kumpata mkandarasi atakayejenga barabara ya kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara yenye urefu wa kilometa 25 kwa njia nne kwa kiwango cha lami. Kwa sehemu ya Mwanza Mjini hadi Kisesa, tayari Serikali imejenga sehemu ya meta 500 kwa njia nne sambamba na ujenzi wa Daraja la Mabatini. Ujenzi wa sehemu iliyobaki utaendelea kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.