Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 379 2026-05-19

Name

Edibily Kinyoma Kazala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Primary Question

MHE. EDIBILY K. KINYOMA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Uvinza – Kasulu na Makere – Nyarugusu Kitanga kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edibily Kazala Kinyoma, Mbunge wa Kasulu Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Uvinza hadi Kasulu na Barabara ya Makere – Nyarugusu hadi Kitanga ni barabara za mkoa zinazohudumiwa na TANROADS Mkoa wa Kigoma. Kwa sehemu ya Uvinza hadi Kasulu yenye urefu wa kilometa 56.8, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imekamilika, na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Aidha, kwa sehemu ya Makere – Nyarugusu hadi Kitanga, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante