Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 379 | 2026-05-19 |
Name
Edibily Kinyoma Kazala
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kasulu Vijijini
Primary Question
MHE. EDIBILY K. KINYOMA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Uvinza – Kasulu na Makere – Nyarugusu Kitanga kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edibily Kazala Kinyoma, Mbunge wa Kasulu Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Uvinza hadi Kasulu na Barabara ya Makere – Nyarugusu hadi Kitanga ni barabara za mkoa zinazohudumiwa na TANROADS Mkoa wa Kigoma. Kwa sehemu ya Uvinza hadi Kasulu yenye urefu wa kilometa 56.8, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imekamilika, na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Aidha, kwa sehemu ya Makere – Nyarugusu hadi Kitanga, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved