Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 380 | 2026-05-19 |
Name
Haran Nyakisa Sanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigamboni
Primary Question
MHE. HARAN N. SANGA aliuliza:-
Je, kuna tofauti gani kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Haran Nyakisa Sanga, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitaalam Daraja la Kigamboni ni Cable Stayed Bridge lenye urefu wa meta 680 ambalo lilijengwa kwa makubaliano maalum kati ya Serikali na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Katika makubaliano hayo, Serikali ilichangia 40% ya gharama za ujenzi na NSSF ilichangia 60%. Aidha, ilikubalika kuwa daraja hilo litakuwa la kulipia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Tanzanite kitaalam ni Extradosed Bridge lenye urefu wa kilometa 1.03 ambalo lilijengwa na Serikali kwa utaratibu wa kawaida na kwa sasa siyo la kulipia. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved