Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 380 2026-05-19

Name

Haran Nyakisa Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. HARAN N. SANGA aliuliza:-

Je, kuna tofauti gani kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Haran Nyakisa Sanga, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitaalam Daraja la Kigamboni ni Cable Stayed Bridge lenye urefu wa meta 680 ambalo lilijengwa kwa makubaliano maalum kati ya Serikali na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Katika makubaliano hayo, Serikali ilichangia 40% ya gharama za ujenzi na NSSF ilichangia 60%. Aidha, ilikubalika kuwa daraja hilo litakuwa la kulipia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Tanzanite kitaalam ni Extradosed Bridge lenye urefu wa kilometa 1.03 ambalo lilijengwa na Serikali kwa utaratibu wa kawaida na kwa sasa siyo la kulipia. Ahsante.