Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Haran Nyakisa Sanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigamboni
Primary Question
MHE. HARAN N. SANGA aliuliza:- Je, kuna tofauti gani kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni?
Supplementary Question 1
MHE. HARAN N. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niseme sijaridhika na majibu ya Mheshimiwa Waziri, kwa sababu haioneshi utofauti wa Daraja la Kigamboni na Daraja la Tanzanite.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoelewa mimi, haya madaraja yote yamejengwa kwa fedha za mkopo, lakini pia Serikali inahusika katika kulipa ile mikopo ambayo imetumika katika kujenga haya madaraja. Ukianza kuangalia Serikali hapa imechangia 40% na NSSF imechangia 60%. Wananchi wa Kigamboni wamekuwa wakilia sana kulingana na tozo zinazotolewa pale darajani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri; je, Serikali iko tayari kutoa 40% kama sehemu ya huduma, ikabaki 60% ili kushusha tozo inayotolewa pale Kigamboni? (Makofi)
Swali la pili, wananchi wa Kigamboni wamechangia sana tozo pale darajani. Nini kauli ya Serikali kufuta tozo kabisa ili waendelee kupita kama wanavyopita watu wa Tanzanite? (Makofi)
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza si vyema kulirudia swali kama lilivyoulizwa. Swali liliulizwa nini tofauti kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Kigamboni?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetoa tofauti hiyo, kwanza kitaalamu kwa maana swali liko hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kuna tofauti gani kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni. Tumetoa tofauti kitaalam kwa maana ya ujenzi ilivyojengwa, lakini pia operations zake zinafanyikaje. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka niliweke wazi hivyo, ili sijui, lakini ndiyo swali lilivyoulizwa.
Sasa naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge. (Makofi/Kicheko)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na maelezo yako, ndiyo maana wakati mwingine tunaruhusu maswali ya nyongeza ambayo yako chini ya Wizara yako, ambayo unaweza kuyajibu. Yale ambayo unaweza kuyajibu, unayajibu hapo, yale ambayo huna majibu basi utayeta majibu baadaye. Kwa hiyo, naomba ujibu maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba sasa hivi mwelekeo wa Serikali na hata mwelekeo wa Dira ya 2050 ni 70% private sector na 30% Serikali na huko ndiyo maana hata leo, tunafikiria kujenga barabara ya kutoka Kibaha kuja Chalinze, kuja Morogoro ikiwezekana mpaka Dodoma kwa Mpango wa PPP ambazo hizo barabara zitakuwa ni za kulipia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa NSSF sisi tunasema tuna kivuko ambacho tunasema ni daraja linalotembea na hili daraja lingine la Kigamboni Serikali iliingia ubia na wenzetu wa NSSF na ndiyo maana likawa la kulipia tangu mwanzo. Hili Daraja la Kigamboni ambalo lililinganishwa tumesema ni kama madaraja mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge maoni hayo tumeyapokea na tutakwenda kuyafanyia kazi, lakini niwajulishe tu Waheshimiwa Wabunge tunakoelekea sasa hivi hata kwenye barabara na nchi zingine sasa hivi ni PPP na ndiyo utaratibu ambao hata Mheshimiwa Rais ametuelekeza tuanze kufanya kazi na wenzetu wa private sector, ahsante.
Name
Asha Juma Feruz
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HARAN N. SANGA aliuliza:- Je, kuna tofauti gani kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni?
Supplementary Question 2
MHE. ASHA J. FERUZ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Waziri pamoja na ufafanuzi ulioutoa uchumi wa watu wa Kinondoni ambalo lipo Daraja la Tanzanite ni mkubwa kuliko uchumi wa watu wa Kigamboni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tozo inayotozwa pale kwenye Daraja la Kigamboni inasababisha nauli kuwa kubwa na kuendelea kuwafanya wananchi wa Kigamboni kuona kupita darajani ni kama adhabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuingia Kigamboni ni pesa na kutoka Kigamboni ni pesa. Ni lini mkataba huo ambao umeingiwa na Serikali pamoja na NSSF utakwisha kwa maana ya kulipa hilo deni na wananchi wa Kigamboni wanufaike na wao waone ni sehemu ya Tanzania na ku-enjoy kupita kwenye daraja? (Makofi)
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge, lakini niseme tu kwa swali la msingi lilivyokuja ningemuomba Mheshimiwa Mbunge muuliza swali atuletee swali la msingi tuliweze kulifanyia kazi ili tuweze kutoa maelezo yanayojitosheleza, ahsante.
Name
Esther Nicholas Matiko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Tarime Mjini
Primary Question
MHE. HARAN N. SANGA aliuliza:- Je, kuna tofauti gani kati ya Daraja la Tanzanite na Daraja la Mwalimu Nyerere Kigamboni?
Supplementary Question 3
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuweza kunipa fursa ya kuuliza swali na tunamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kuweza kutoa utofauti kati ya madaraja yale mawili.
Swali langu ni kutaka kujua Serikali imejifunza nini kutokana na uendeshaji wa madaraja haya mawili ili kuweza kuongeza ufanisi kwenye miundombinu mingine ya kimkakati ambayo mnajenga nchini?
Name
Prof. Kitila Alexander Mkumbo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ubungo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukishakuwa na private sector kwanza una uwezo wa kufanya miradi mingi kwa sababu private sector wanachangia na wewe unachangia na kwa maana hiyo ndiyo maana nadhani utaona hata kwenye maboma Serikali tunasema wananchi wakishachangia tunaweza tukajenga maboma 30 badala ya kujenga maboma 15 kwa sababu kuna nguvu ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili ndiyo maana wenzetu maana yake hili siyo suala jipya labda sisi ndiyo tumeanza na wengine wanasema tumechelewa, ndiyo maana miradi mingi sasa hivi tunasema tutakwenda kwenye PPP na huo ndiyo mtazamo wa Serikali. Ahsante.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri tunakushukuru kwa kwa majibu yako kwa maswali ya Waheshimiwa Wabunge. Nilikuwaona Waziri wa Mipango, Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo.
WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwanza nataka nichukue nafasi kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri anavyojibu maswali kwa umahiri wa hali ya juu sana kwa sekta ambayo amei-master sana tangu awe Mheshimiwa Naibu Waziri katika Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu nijibu swali na niweke maelezo ya msingi na swali la Mheshimiwa Matiko ni la muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya fundisho ambalo tunalipata tunapoelekea kwenye ushirikiano wa sekta binafsi na sekta ya umma, ni kwamba ni muhimu tutoe elimu mapema kwa wananchi juu ya nature ya mradi wenyewe. Mradi wa Daraja la Kigamboni kuanzia mwanzo ilikuwa ni kwamba huu ni mradi ambao utajengwa kwa fedha zitakazotolewa na NSSF na utakapokamilika ni kwamba fedha zitarudi kwa wananchi kulipa fee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Tanzanite tumelijenga kwa fedha za mkopo nafuu (concessional loan) na mule ndani mpaka ukupe concessional loan maana yake ni kwamba siyo business tungeweka tangu mwanzo kwamba wananchi watalipa isingekuwa concessional loan.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ambacho tunajifunza hapa ni kwamba lazima sisi Serikali tutoe maelezo ya kina kuhusu mradi unapoanza. Hapa tunajiandaa kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri tunajiandaa kutekeleza mradi wa PPP wa barabara ya Dar es Salaam - Chalinze kuja huku kwa PPP maana yake lazima tuambie wananchi kwamba mradi huu utajengwa kwa PPP na kwamba fedha ambazo zitajenga zitarudishwa kwa njia ya kulipa.
Kwa hiyo, watakapokuwa wanapita siyo tumejenga leo kesho wakasema ah! kwa nini tunalipia, kwa hiyo nadhani kitu kikubwa hapa ni kwamba ni elimu kwa umma na tutaongeza jitihada katika eneo hilo. Ahsante sana. (Makofi)