Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Water and Irrigation Wizara ya Maji 381 2026-05-19

Name

Twaha Said Mwakioja

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. TWAHA S. MWAKIOJA aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya utafiti wa vyanzo vya uhakika vya maji Tarafa ya Maramba, Wilaya ya Mkinga ili kutatua changamoto ya maji kwa wananchi?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Said Mwakioja, Mbunge wa Jimbo la Mkinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza utafiti wa maji chini ya ardhi katika maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa maji Wilayani Mkinga, mkoani Tanga ikiwemo baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Maramba. Utafiti huo umeonesha uwepo wa maji chini ya ardhi katika vijiji vinne vya tarafa hiyo ambavyo ni Kichangani, Gombero, Maramba A na Matemboni, sanjali na Kijiji cha Mkota kilichopo Kata ya Mwakijembe wilayani humo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa taratibu za kuanza uchimbaji wa visima virefu katika maeneo yaliyobainishwa zinaendelea. Aidha, Serikali itaendelea na zoezi la utafiti wa vyanzo vingine vya maji katika maeneo yenye changamoto wilayani Mkinga ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa wilaya nzima ikiwemo wale wa Tarafa ya Maramba.