Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Finance Wizara ya Fedha 383 2026-05-19

Name

Lucy Edward Mwakyembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni?

Name

Mshamu Ali Munde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. ENG. MSHAMU A. MUNDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Edward Mwakyembe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Fedha imekuwa ikitenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya kugharamia ulipaji wa madeni ya wakandarasi, wazabuni na watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2025/2026, shilingi bilioni 700 zilitengwa ambapo hadi Februari, 2026 jumla ya shilingi bilioni 477.6 zimetolewa. Kadhalika, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 800 katika mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kugharamia ulipaji wa madeni yaliyohakikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa suala la madeni ya wakandarasi na wazabuni linadhibitiwa, Serikali inaendelea kutoa maelekezo kwa Maafisa Masuuli kupitia waraka mbalimbali za utekelezaji wa bajeti na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti katika mwaka husika. Maelekezo ya Serikali ni kama yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafungu kutenga bajeti kwa ajili ya ulipaji wa madeni ya wakandarasi, wazabuni na watumishi, lakini pia Maafisa Masuuli kutumia mifumo ya kudhibiti matumizi hali kadhalika kuhakikisha kuwa mchakato wowote wa ununuzi unaanzishwa baada ya kujiridhisha uwepo wa bajeti na uhakika wa upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha ninaomba kuwasilisha. (Makofi)