Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Finance | Wizara ya Fedha | 383 | 2026-05-19 |
Name
Lucy Edward Mwakyembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni?
Name
Mshamu Ali Munde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. ENG. MSHAMU A. MUNDE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Edward Mwakyembe, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Fedha imekuwa ikitenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya kugharamia ulipaji wa madeni ya wakandarasi, wazabuni na watumishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2025/2026, shilingi bilioni 700 zilitengwa ambapo hadi Februari, 2026 jumla ya shilingi bilioni 477.6 zimetolewa. Kadhalika, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 800 katika mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kugharamia ulipaji wa madeni yaliyohakikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa suala la madeni ya wakandarasi na wazabuni linadhibitiwa, Serikali inaendelea kutoa maelekezo kwa Maafisa Masuuli kupitia waraka mbalimbali za utekelezaji wa bajeti na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti katika mwaka husika. Maelekezo ya Serikali ni kama yafuatayo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, mafungu kutenga bajeti kwa ajili ya ulipaji wa madeni ya wakandarasi, wazabuni na watumishi, lakini pia Maafisa Masuuli kutumia mifumo ya kudhibiti matumizi hali kadhalika kuhakikisha kuwa mchakato wowote wa ununuzi unaanzishwa baada ya kujiridhisha uwepo wa bajeti na uhakika wa upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved