Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Lucy Edward Mwakyembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni?
Supplementary Question 1
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na ninamshukuru sana Naibu Waziri kaka yangu Mheshimiwa Munde kwa majibu mazuri ya Serikali pamoja na mikakati ambayo imewekwa kwa ajili ya ulipwaji madeni hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua Serikali inaendelea kutekeleza upatikanaji wa ajira milioni nane ambazo zimeainishwa kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi mpaka kufikia mwaka 2030 na pia niwapongeze sekta binafsi ambapo zinavyoongeza kuongeza ajira za vijana wa kike na kiume katika kutekeleza Ilani hiyo ya Chama Cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuuliza swali moja la nyongeza. Serikali ina mpango gani katika kusimamia madeni hayo yasiongezeke hasa ya wazabuni na wakandarasi wazawa ili kuendelea kulinda mitaji yao na wao hao kuendelea kulinda ajira za vijana wa kike na wa kiume, lakini pia na kuhakikisha madeni ya watumishi yanalipwa na madeni ya watumishi hayaongezeki? Ahsante.
Name
Mshamu Ali Munde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. ENG. MSHAMU A. MUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lucy Edward Mwakyembe, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli madeni ya wazabuni na wakandarasi pamoja na watumishi ni kero ambayo Wizara imeipata, lakini pia kupitia Wabunge mbalimbali jambo hili limekuwa likiongelewa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuliona hilo, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kesho siku ya Jumatano, tarehe 20 Mei itakutana na Wizara ya Fedha katika kutafakari na kuhakikisha kwamba madeni hasa hasa ya wazabuni na wakandarasi wa ndani yanaweza kulipwa ili uchumi uweze kuzunguka lakini pia vijana ambao wamefanya kazi kwenye miradi hiyo waweze kupata kujikimu na kuinua vipato na uchumi wa mmoja mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Name
Lucy Thomas Mayenga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni?
Supplementary Question 2
MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la madeni Serikalini ni suala ambalo limeumiza watu wengi sana, kwanza kwa sababu uhakiki wa madeni hauna kipindi maalum kwamba uhakiki wa madeni utafanyika ndani ya mwaka mmoja, ndani ya miaka miwili, ndani ya miaka mitatu. Kwa hiyo, wale wakopaji ambao walifanya miradi hii ya Serikali kwa nia njema wamekuwa wakiumizwa kwa interest za mabenki na wengi wamekuwa wakilalamika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Wizara hii ya Fedha isikae na hao Maafisa Masuuli, kwa sababu hata hicho kinachosemwa kuanzisha miradi mipya baada ya ile miradi mingine kulipwa hakifanyiki. Kwa nini Wizara hii isingekuwa inakaa inawasaidia hawa ambao wanadai kuweza kuongea na mabenki walau kuangalia njia sahihi za kuwasaidia ikiwemo kupatana kwenye suala zima la interest badala ya kutoa maelekezo ambayo kwa kweli yamekuwa akiumiza sana watu? Ahsante. (Makofi)
Name
Mshamu Ali Munde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. ENG. MSHAMU A. MUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Lucy kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninatambua ni kweli wakandarasi na wazabuni wamekuwa wakiumia sana kutokana na kutolipwa kwa wakati ambazo wamezifanya katika miradi ya maendeleo ambayo inahudumia wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uhakiki kwa sasa kama nilivyotangulia kusema umefanyika kupitia Maafisa Masuuli, lakini pia Wizara za Kisekta na baadhi ya taarifa zilizo nyingi tumeshazipata na ndio maana kesho tuna kikao mahsusi kwa ajili ya kupitia orodha zote za madeni ili tuweze kupanga mkakati ambao utaenda kupunguza kabisa na kama sio kuondoa kwa kiwango kikubwa madeni yote ambayo wazabuni wanaidai Serikali ili mwisho wa siku twende kuangalia miradi mipya badala ya kuhangaika na madeni ambayo mpaka sasa hivi wazabuni na wakandarasi wanadai.
Name
Tinnar Andrew Chenge
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni?
Supplementary Question 3
MHE. TINNAR A. CHENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali italipa madeni ya wakandarasi wa Wilaya ya Meatu ambayo yameshafanyiwa uhakiki na kutumwa TAMISEMI na Hazina kwa ajili ya malipo? Nashukuru sana. (Makofi)
Name
Mshamu Ali Munde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. ENG. MSHAMU A. MUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nijibu kwa ujumla.
Mheshimiwa Tinnar Chenge ninashukuru sana kwa swali lako lakini niseme wazi kwamba amesema madeni ya Wilaya ya Meatu. Hayo ni madeni jumuishi ambayo haijulikani sasa ni wakandarasi wa Wizara ya Maji au miradi ya barabara au ni miradi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaongea naye nje ya forum hii ili kupata uhakika na specific hoja yake iko vipi ili tuweze kumjibu kiuhalisia kutokana na swali ambalo atakuwa ametupatia nje ya kikao hiki. (Makofi)
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni?
Supplementary Question 4
MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante ninakushukuru kwa nafasi.
Swali langu linasema je, Serikali imeweka mikakati gani katika kuongeza uwazi na uwajibikaji kwenye mchakato wa ulipaji wa madeni ya wakandarasi na wazabuni?
Name
Mshamu Ali Munde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. ENG. MSHAMU A. MUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la dogo la nyongeza la Mheshimiwa Janeth kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotangulia kusema kuhusiana na uwazi na uwajibikaji Kamati ya Kudumu ya Bajeti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kesho linapitia taarifa zote za madeni ya wakandarasi na wazabuni. Kamati hiyo wajumbe wake ni Wabunge, Wabunge ambao wanawakilisha wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, taarifa ambazo tunazipeleka sisi kama Wizara ya Fedha inaenda kuwekwa wazi mbele ya Kamati ambayo mwisho wa siku tunaonesha ule uwazi wa kwamba madeni yote ambayo yamehakikiwa, ambayo hayajahakikiwa kiasi gani tunaenda kulipa na mkakati gani tunaenda kuufanya ili kulipa madeni hayo. Huo ndio uwazi na uwajibikaji ambao tunaongelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.