Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 384 | 2026-05-19 |
Name
Saashisha Elinikyo Mafuwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hai
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kudhibiti watoa elimu ya afya na aina ya ulaji mitandaoni bila kuwa na taaluma inayotambulika jambo linalowachanganya wananchi?
Name
Dr. Florence George Samizi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampenda kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua ongezeko la watu binafsi au wataalamu wanaotoa elimu au ushauri wa afya na lishe kupitia mitandao ya kijamii, hali inayoweza kupotosha na kuhatarisha afya za wananchi. Hii inatokana na kukua kwa uelewa wa masuala ya lishe, afya, utandawazi na ongezeko la vyombo vya kutolea habari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza Sheria ya Afya ya Jamii ya Mwaka 2009 Kifungu Namba 173(1) ambacho kinamtaka mtoa maudhui, mada au matangazo yanayohusu afya ya jamii kupata kibali kutoka kwa Waziri wa Afya au Afisa aliyeidhinishwa na Waziri. Kushindwa au kwenda kinyume na sheria hii mtoa maudhui au mtoa mada atachukuliwa hatua za kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved