Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 32 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 385 2026-05-19

Name

Ester Edwin Malleko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza upatikanaji wa mbegu bora na kwa bei nafuu nchini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuongeza uzalishaji wa mbegu nchini kwa kutenga maeneo kwa ajili ya kuanzisha mashamba mapya ya kuzalisha mbegu, kuhamasisha kampuni binafsi za mbegu kuingia mikataba maalum na ASA ili kuzalisha mbegu bora kwa kutumia mashamba ya Serikali, na kuhamasisha uzalishaji wa mbegu za daraja la kuazimiwa ubora kwa maana ya Quality Declared Seeds – QDS kwa wakulima wadogo ili kuwaruhusu wakulima kuzalisha na kuuza mbegu zinazofaa kwenye maeneo husika kwa bei nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuimarika kwa uzalishaji wa mbegu nchini kutasababisha kupungua kwa ongezeko la bei linalotokana na uagizaji wa mbegu nje ya nchi. Vilevile, Wizara inaendelea kutekeleza azma ya Serikali ya kutoa ruzuku ya mbegu bora ya mazao ya kimkakati.