Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 32 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 385 | 2026-05-19 |
Name
Ester Edwin Malleko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza upatikanaji wa mbegu bora na kwa bei nafuu nchini?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuongeza uzalishaji wa mbegu nchini kwa kutenga maeneo kwa ajili ya kuanzisha mashamba mapya ya kuzalisha mbegu, kuhamasisha kampuni binafsi za mbegu kuingia mikataba maalum na ASA ili kuzalisha mbegu bora kwa kutumia mashamba ya Serikali, na kuhamasisha uzalishaji wa mbegu za daraja la kuazimiwa ubora kwa maana ya Quality Declared Seeds – QDS kwa wakulima wadogo ili kuwaruhusu wakulima kuzalisha na kuuza mbegu zinazofaa kwenye maeneo husika kwa bei nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuimarika kwa uzalishaji wa mbegu nchini kutasababisha kupungua kwa ongezeko la bei linalotokana na uagizaji wa mbegu nje ya nchi. Vilevile, Wizara inaendelea kutekeleza azma ya Serikali ya kutoa ruzuku ya mbegu bora ya mazao ya kimkakati.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved