Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 160 2026-04-22

Name

Christina Solomon Mndeme

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHRISTINA S. MNDEME aliuliza: -

Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inawafikia Wanawake wote wenye uhitaji wa Mikopo katika Mkoa wa Tabora?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Solomon Mndeme, Mbunge wa viti maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuhakikisha kwamba wanawake wenye sifa katika Mkoa wa Tabora wanafikiwa na mikopo ya 10% kwa kuongeza fedha zinazotengwa kwa vikundi vya wanawake. Katika Mkoa wa Tabora, kiasi cha mikopo kwa wanawake kimeongezeka kutoka shilingi bilioni 1.54 mwaka 2020/2021 hadi shilingi bilioni 4.80 mwaka 2024/2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Maafisa Maendeleo ya Jamii katika halmashauri za Mkoa wa Tabora Serikali inaendelea kuwasaidia wanawake kuunda na kusajili vikundi, kupata mafunzo ya ujasiriamali na kuandaa miradi yenye tija ili waweze kukidhi vigezo vya kupata mikopo. Kutokana na hatua hizo, vikundi vya wanawake vilivyosajiliwa na kupewa mikopo vimeongezeka kutoka vikundi 234 mwaka 2020/2021 hadi vikundi 532 mwaka 2024/2025, huku vikundi vilivyopatiwa mafunzo vikiongezeka kutoka 1,718 hadi 5,907 katika kipindi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia inaendelea kutumia mfumo wa WEZESHA Portal katika usajili na usimamizi wa mikopo. Aidha, Serikali imezielekeza halmashauri zote kutangaza fursa hizo kwa uwazi kupitia mbao za matangazo, mikutano ya hadhara na vyombo vya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuongeza uhamasishaji na kuwajengea uwezo wanawake wanufaike zaidi na mikopo hiyo.