Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 14 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 160 | 2026-04-22 |
Name
Christina Solomon Mndeme
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CHRISTINA S. MNDEME aliuliza: -
Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inawafikia Wanawake wote wenye uhitaji wa Mikopo katika Mkoa wa Tabora?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Solomon Mndeme, Mbunge wa viti maalumu kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuhakikisha kwamba wanawake wenye sifa katika Mkoa wa Tabora wanafikiwa na mikopo ya 10% kwa kuongeza fedha zinazotengwa kwa vikundi vya wanawake. Katika Mkoa wa Tabora, kiasi cha mikopo kwa wanawake kimeongezeka kutoka shilingi bilioni 1.54 mwaka 2020/2021 hadi shilingi bilioni 4.80 mwaka 2024/2025.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Maafisa Maendeleo ya Jamii katika halmashauri za Mkoa wa Tabora Serikali inaendelea kuwasaidia wanawake kuunda na kusajili vikundi, kupata mafunzo ya ujasiriamali na kuandaa miradi yenye tija ili waweze kukidhi vigezo vya kupata mikopo. Kutokana na hatua hizo, vikundi vya wanawake vilivyosajiliwa na kupewa mikopo vimeongezeka kutoka vikundi 234 mwaka 2020/2021 hadi vikundi 532 mwaka 2024/2025, huku vikundi vilivyopatiwa mafunzo vikiongezeka kutoka 1,718 hadi 5,907 katika kipindi hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia inaendelea kutumia mfumo wa WEZESHA Portal katika usajili na usimamizi wa mikopo. Aidha, Serikali imezielekeza halmashauri zote kutangaza fursa hizo kwa uwazi kupitia mbao za matangazo, mikutano ya hadhara na vyombo vya mawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuongeza uhamasishaji na kuwajengea uwezo wanawake wanufaike zaidi na mikopo hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved