Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 14 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 161 | 2026-04-22 |
Name
Revocatus Chipando Clayton
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Mjini
Primary Question
MHE. CLAYTON R. CHIPANDO aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza mtandao wa Barabara za lami Kigoma Mjini kwa kuongeza bajeti?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Clayton Revocatus Chipando, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji hadi mwaka wa fedha 2020/2021 ilikuwa inapokea Bajeti ya Matengenezo ya barabara na madaraja jumla ya shilingi bilioni 1.6 kwa mwaka. Kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 mpaka 2025/2026, bajeti iliongezeka hadi kufikia shilingi bilioni 3.2 kwa mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo wa Benki ya Dunia kupitia Mradi wa TACTIC Awamu ya Kwanza inatekeleza Mradi wa Ujenzi wa Barabara za kilometa 9.4, Mitaro Mikubwa ya Maji ya Mvua kilometa 5.4, Soko kuu la Mwanga pamoja na Soko la Samaki la Katonga katika Manispaa ya Kigoma Ujiji. Utekelezaji wa mradi huu utaongeza mtandao wa Barabara za lami Kigoma Mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuujengea uwezo wa kibajeti wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini ili uweze kutekeleza Ujenzi wa Barabara za tabaka la lami kwa awamu kote nchini ikiwemo katika Manispaa ya Kigoma.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved