Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 14 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 166 2026-04-22

Name

Chief Thomas Mgonto Kitima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ikungi Mashariki

Primary Question

MHE. THOMAS M. KITIMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itahakikisha kila kijiji nchini kinapata mawasiliano ya kimtandao na kuwepo kwa minara ili kurahisisha mawasiliano hayo?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Thomas Mngoto Kitima, Mbunge wa Jimbo la ikungi Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa huduma za mawasiliano ya uhakika katika kila kijiji nchini kama msingi wa kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hasa katika zama hizi za uchumi wa kidijiti. Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kushirikiana na taasisi zilizo chini ya Wizara pamoja na Sekta Binafsi, imeendelea kupanua miundombinu ya mawasiliano ikiwemo ujenzi wa minara ya simu, hususan katika maeneo ya vijijini ambayo bado kuna changamoto ya mawasiliano ya simu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeandaa Mpango Mkakati Mahsusi wa Ujenzi wa Minara kwa Kipindi cha Miaka Mitano (2025 – 2030). Mpango huu unalenga kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vijiji vyote nchini vinapata huduma za mawasiliano mbadala ili kuwezesha wananchi kupata huduma ya mawasiliano na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utekelezaji wa mpango huu, mwezi Disemba, 2025 Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa wote, ilikamilisha Mradi wa Awamu ya Nane ya Ujenzi wa Minara 758 nchini. Utekelezaji wa awamu ya tisa ya ujenzi wa minara 636 unaendelea na utakamilika mwezi Disemba, 2026.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, UCSAF inaendelea na awamu ya 10 ya ujenzi wa minara 287 ambayo mikataba yake ilisainiwa Disemba, 2025. Hatua hii inalenga kuongeza upatikanaji wa huduma za Mawasiliano katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na kuboresha huduma kwa wananchi.