Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Chief Thomas Mgonto Kitima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ikungi Mashariki

Primary Question

MHE. THOMAS M. KITIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itahakikisha kila kijiji nchini kinapata mawasiliano ya kimtandao na kuwepo kwa minara ili kurahisisha mawasiliano hayo?

Supplementary Question 1

MHE. THOMAS M. KITIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. kwa kuwa karibia kata nyingi hazina mawasiliano, Mfano vijiji katika Kata ya Mang’onyi, Ntuntu, Misuhaa, Kikio ambapo kuna maeneo kama Mnane, Kundi, pamoja na Makumi, ambao hawana kabisa mawasiliano; na hata mimi nikienda kwenye ziara huwa nikifika huko ni kama nipo gizani, au nimepotea na siwezi kupatikana; je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuwapatia hawa watu mawasiliano kwa kuwajengea minara, hasa hasa katika maeneo yenye huduma za kijamii kama shule ili yawepo mawasiliano na iweze kufanya miradi ya Kitaifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kijiji ninachotoka kinaitwa Siuyi na nikiwa kijijini huwa ninalazimika kwenda kijiji cha jirani ambacho kinaitwa Makiungu, ili tu nipate mawasiliano. Mara nyingine huwa ninalazimika kutokufika kijijini, nilale mjini ili mradi tu nisikose taarifa za Kitaifa. Kwa mfano, Mheshimiwa Rais ana jambo la Kitaifa, kwa hiyo, ninalazimika kukaa mjini ili tu niweze kupata mawasiliano, kwa kuwa kijiji ninachotoka hakuna mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itaona umuhimu hiki Kijiji cha Siuyi kipate mawasiliano ya kutosha? Kwa kuwa mimi Mbunge wao ninatoka pale, wakiona hata Mbunge hana mawasiliano, itakuwa siyo jambo zuri. (Makofi)

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Wizara tumepokea changamoto ya Mheshimiwa Mbunge. Ninaomba nimwelekeze Mkurugenzi Mkuu wa UCSAF aende jimboni kwa Mheshimiwa kufanya tathmini ya kina kuhusu tatizo hili la mawasiliano na kuchukua hatua za dharura kulifanyia utatuzi kwa kadri itakavyowezekana. (Makofi)