Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 14 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 167 2026-04-22

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa vihenge vya Kisasa (maghala) vya kutunzia mazao vilivyopo eneo la TAZARA Isangi Mbozi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Ujenzi wa Vihenge vya Kisasa (maghala) vya kutunzia mazao vilivyopo eneo la TAZARA Isangi Mbozi ni mojawapo ya miradi ya ujenzi wa vihenge na maghala ya kisasa unaotekelezwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula Nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vihenge hivyo ulikuwa ukitekelezwa na Kampuni ya Feerum S. A. ambayo ilishindwa kukamilisha kazi hiyo kwa wakati na hatimaye Serikali ilisitisha mkataba wake ukiwa umefikia 74% ya utekelezaji mnamo Oktoba, 2024. Baada ya hatua hiyo, mkandarasi mpya Unia Araj amepatikana na anatarajiwa kukamilisha kazi hiyo ifikapo Juni, 2027.