Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 14 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 168 | 2026-04-22 |
Name
Daniel Awack Tlemai
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karatu
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: -
Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya shilingi bilioni 4.5 kwa wananchi wa Mji wa Karatu ili waweze kupata huduma ya uhakika ya majisafi?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Awack, Mbunge wa Jimbo la Karatu, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji inayolenga kuboresha huduma ya majisafi na salama kwa wananchi wa Karatu Mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha kuanzia mwaka wa fedha 2024/2025 hadi sasa, jumla ya shilingi bilioni 1.742 zimetolewa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Karatu (KARUWASA) ikiwa ni sehemu ya ahadi ya Serikali ya kuboresha huduma ya maji katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizo zimewezesha kukamilisha utekelezaji wa miradi ya maji Ayalabe, Bwawani Namba tatu sambamba na uchimbaji wa visima vitatu vya Endoro, Maliasili pamoja na Tom III ambapo kwa pamoja vina uwezo wa kuzalisha maji lita 200,000 kwa saa. Vilevile, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya maji Karatu Mjini wenye thamani ya shilingi 864,822,827.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutoa kipaumbele cha kupeleka fedha za utekelezaji wa miradi ya maji katika Jimbo la Karatu kadiri fedha zinavyopatikana ili kuhakikisha miradi inayoendelea inakamilika.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved