Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 511 2026-06-04

Name

Twaha Said Mwakioja

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. TWAHA S. MWAKIOJA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakarabati madarasa chakavu na kujenga madarasa mapya katika Shule za Msingi Jimbo la Mkinga?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Said Mwakioja, Mbunge wa Jimbo la Mkinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kufanya ukarabati wa shule katika Wilaya ya Mkinga ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 mpaka kufikia mwaka 2025/2026, Serikali imepeleka jumla ya shilingi bilioni 2.78 katika Wilaya ya Mkinga kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili mpya za msingi, madarasa 82 katika shule 35 chakavu za msingi na ukarabati wa shule tatu chakavu za msingi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 275.2 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa matatu, matundu ya vyoo 94 katika shule 19 za msingi katika Jimbo la Mkinga.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kujenga madarasa na kukarabati shule za msingi chakavu nchini zikiwemo shule za Jimbo la Mkinga. Naomba kuwasilisha.