Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 43 | Planning and Investment | Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji | 512 | 2026-06-04 |
Name
Chief Thomas Mgonto Kitima
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ikungi Mashariki
Primary Question
MHE. THOMAS M. KITIMA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050?
Name
Prof. Kitila Alexander Mkumbo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ubungo
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA) K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji nami naomba kujibu swali la Mheshimiwa Thomas Mgonto Kitima, Mbunge wa Jimbo la Ikungi Mashariki:-
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Dira 2050 utaanza rasmi tarehe 01 Julai, 2026 kufuatia kufikia ukomo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo yam waka 2025 tarehe 30 Juni, 2026. Utekelezaji huu ni baada ya kuzinduliwa kwa Dira 2050 tarehe 17 Julai, 2025 na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kuandaa nyenzo mbalimbali za utekelezaji wa dira hiyo, zikiwemo: -
(i) Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu (Long Term Perspective Plan);
(ii) Mpango wa Nne wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa mwaka 2026/2027 hadi 2030/2031;
(iii) Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Miradi ya Maendeleo;
(iv) Mwongozo wa Kitaifa wa Uidhinishaji wa Miradi ya Maendeleo; na
(v) Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Mwaka Mmoja wa 2026/2027 (Annual Development Plan).
Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilika kwa nyenzo hizo, Serikali itaanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 sanjari na kutoa elimu kwa umma kuhusu mfumo na utaratibu utakaotumika katika utekelezaji wa dira hiyo, pamoja na mipango ya maendeleo ya miaka mitano na ya mwaka mmoja. Aidha, utekelezaji wa nyenzo hizo utafuatiliwa na kupimwa kidijitali kupitia mfumo wa e-Delivery (Mfumo wa Kitaifa wa Usimamizi wa Mipango na Miradi ya Maendeleo) kwa lengo la kuimarisha ufanisi, uwajibikaji na upatikanaji wa taarifa na takwimu za utekelezaji kwa wakati halisi.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved