Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 43 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 513 2026-06-04

Name

Mgore Miraji Kigera

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. MGORE M. KIGERA aliuliza: -

Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mwekezaji aliyeonesha nia ya kuwekeza Hoteli ya New Musoma ambayo ni alama ya Mji na Mkoa wa Mara?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mgore Miraji Kigera, Mbunge wa Musoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shirika la Reli linaendelea kuboresha nyumba na majengo ya biashara pamoja na hoteli zinazomilikiwa na shirika ikiwemo Hoteli ya Musoma. Aidha, TRC imejidhatiti katika kuhakikisha kwamba inashirikisha sekta binafsi katika kufanya uwekezaji wa hoteli hii ili kuleta tija na kuongeza mapato ya shirika.

Mheshimiwa Spika, TRC ilipokea mwekezaji ambaye ameonesha nia ya kuwekeza katika Hoteli ya Musoma. Aidha, shirika limemtaka mwekezaji kuwasilisha andiko la mradi, pamoja na michoro ya maboresho anayotaraji kuyafanya. Pindi atakapokamilisha uwasilishaji wa nyaraka hizo hatua za kuendelea na majadiliano zitaanza.