Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 43 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 513 | 2026-06-04 |
Name
Mgore Miraji Kigera
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Musoma Mjini
Primary Question
MHE. MGORE M. KIGERA aliuliza: -
Je, Serikali imefikia wapi kuhusu mwekezaji aliyeonesha nia ya kuwekeza Hoteli ya New Musoma ambayo ni alama ya Mji na Mkoa wa Mara?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mgore Miraji Kigera, Mbunge wa Musoma Mjini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Shirika la Reli linaendelea kuboresha nyumba na majengo ya biashara pamoja na hoteli zinazomilikiwa na shirika ikiwemo Hoteli ya Musoma. Aidha, TRC imejidhatiti katika kuhakikisha kwamba inashirikisha sekta binafsi katika kufanya uwekezaji wa hoteli hii ili kuleta tija na kuongeza mapato ya shirika.
Mheshimiwa Spika, TRC ilipokea mwekezaji ambaye ameonesha nia ya kuwekeza katika Hoteli ya Musoma. Aidha, shirika limemtaka mwekezaji kuwasilisha andiko la mradi, pamoja na michoro ya maboresho anayotaraji kuyafanya. Pindi atakapokamilisha uwasilishaji wa nyaraka hizo hatua za kuendelea na majadiliano zitaanza.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved