Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 43 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 514 2026-06-04

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Bwawa la Mayuyu na Skimu ya Umwagiliaji - Korogwe Vijijini?

Name

Daniel Godfrey Chongolo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Answer

NAIBU WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji nchini ikiwemo katika Wilaya ya Korogwe ambapo kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zinaendelea katika Skimu za Kwamngumi, Magoma, Mapangoni na Kwagunda ambapo usanifu huo unajumuisha Mabwawa ya Magoma na Mapangoni (Mayuyu) yaliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe. Usanifu wa mabwawa hayo umefikia wastani wa 40% kwa usanifu wa Bwawa la Magoma na 73.6% kwa usanifu wa Bwawa Mapangoni na unatarajiwa kukamilika ifikapo Novemba, 2026. Baada ya usanifu wa mabwawa hayo kukamilika utajumuishwa kwenye mpango wa ujenzi wa miradi ya umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali inaendelea na ujenzi wa skimu za umwagiliaji katika Skimu za Mkomazi na Chekelei zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ikihusisha ujenzi wa Mabwawa ya Mkomazi na Chekelei ambapo utekelezaji wake umefikia 96.4% kwa Bwawa la Mkomazi na 10% kwa Bwawa la Chekelei. Ujenzi wa Bwawa la Mkomazi unatarajiwa kukamilika Septemba, 2026 na ujenzi wa Bwawa la Chekelei unatarajiwa kukamilika mwezi Februari, 2027.

Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa miradi hiyo kutanufaisha wakulima 20,000 katika Vijiji vya Manga Mtindiro, Goha, Kwenangu, Magila, Mkumbara, Mazinde Mheza, Mazinde Bagamoyo, Mabogo, Kasiga, Mlembule, Magila Gereza, Mombo, Makuyuni, Kwasunga, Chekelei, Chepete, Madumu na Madala.