Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 43 | Finance | Wizara ya Fedha | 515 | 2026-06-04 |
Name
William Kafiti Kafiti
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ilemela
Primary Question
MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha Kanuni za Bima za Kilimo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali?
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kafiti William Kafiti, Mbunge wa Jimbo la Ilemela, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utafiti kuhusu bima katika mnyororo wa kilimo yaani mazao, mifugo, misitu na uvuvi ili kwa pamoja na mambo mengine kuwa na kanuni zinazovutia uwekezaji katika bima ya kilimo na kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima ili kupata huduma za bima kwa urahisi na haraka. Ni mpango wa Serikali kukamilisha uandaaji wa kanuni hizi katika kipindi cha mwaka 2026/2027. Naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved