Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
William Kafiti Kafiti
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ilemela
Primary Question
MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Kanuni za Bima za Kilimo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali?
Supplementary Question 1
MHE. KAFITI W. KAFITI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na sasa naomba niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu na umeajiri wananchi wengi katika nchi yetu ya Tanzania, kwa hiyo suala la kinga ya bima kwao ni ulinzi mkubwa juu ya kilimo wanachokifanya, na kwa kuwa suala hili limeshachukua muda mrefu, sasa nini kauli ya Serikali juu ya ukamilishwaji wa kanuni hizi ili ziweze kusaidia wananchi wetu? (Makofi)
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nikiri, ni kweli kabisa kilimo ndicho kimeajiri Watanzania wengi sana ambao wanajipatia kipato na kulingana na umuhimu wake na ndiyo maana kiukweli tumechukua muda mrefu ili kujiridhisha kwamba hizi kanuni zitakuwa rafiki kwa wakulima na Watanzania wote ambao wanajihusisha na kilimo. Kwa maana hiyo, kama ambavyo nimeweza kujibu kwenye jibu langu la msingi, mwaka huu wa fedha utakaonza 2026/2027 ndipo tunaenda kukamilisha utafiti huu na kanuni hizo zitaanza kutumika. Naomba kuwasilisha.
Name
Kenneth Ernest Nollo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bahi
Primary Question
MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Kanuni za Bima za Kilimo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali?
Supplementary Question 2
MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na nia njema ya Serikali ya kutaka kuleta bima katika sekta ya kilimo na mifugo, lakini nataka niulize, kwenye suala zima la mifugo; ni masuala gani makubwa ambayo, kwanza yanaleta tatizo kubwa la kutopata bima ili kabla ya kufikiria kutengeneza kanuni mmeyaona mrekebishe ili kwamba hata mtu akitaka kupata bima isiwe na risk kubwa zaidi katika suala hilo?
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza, kuja na kanuni hizi maana yake hata sisi wenyewe kama Wizara, kuja na hii bima ya kilimo tumeona kabisa kwamba kuna umuhimu wake. Ndiyo maana kabla ya kuingia, kwa maana ya kuleta kanuni, tukasema tufanye utafiti kwa kushirikiana na wadau ili tuweze kupata maoni yao nabaada sasa ya kupata maoni yao, tukishakamilisha, ili tuje sasa na bima ambayo, sasa itakuwa na utekelezaji ambao ni imara.
Mheshimiwa Spika, kwa namna hiyo, nipende tu kumhakikishia Mbunge ya kwamba hapo awali hatukuwa na bima hizo, lakini baada ya kuona sasa kuna umuhimu wa kuwa na bima hizo za kilimo ikiwemo ufugaji na ndiyo maana tukasema kwa haraka na kuchukua jukumu la haraka kufanya utafiti na kwa sababu tuko mwishoni, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba baada tu ya kumaliza, tutafanya mipango mingine na kwa kukaribisha maoni mengine ya wadau, ili kama pengine kanuni zile zina mapungufu, basi tuweze kuzirekebisha kulingana na maoni mengine mapya ya wadau.
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana.
Name
Fadhili Fabian Ngajilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iringa Mjini
Primary Question
MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Kanuni za Bima za Kilimo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali?
Supplementary Question 3
MHE. FADHILI F. NGAJILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, nilitaka kuuliza kwamba, kwenye hizi kanuni ambazo zitaundwa kwa ajili ya bima ya mifugo na kilimo; je, wakulima wadogo au wafugaji wadogo wameshashirikishwa kwa namna gani, kwa sababu tuna tatizo kwenye ufugaji, wafugaji wetu wanapoteza sana mifugo yao kutokana na magonjwa na ajali ambazo zinatokea. Je, sasa wanaingizwa vipi katika mfumo huo wa kupata hizo bima ili tuokoe mitaji hii ya wafugaji wadogo? (Makofi)
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimhakikishie Mbunge kwamba wakulima hawa wadogo ambao anawazungumzia na wao pia ni miongoni mwa wadau ambao tayari tumekwishawashirikisha kuhusu bima hii ya kilimo. Wao wametoa maoni yao na kwa kipindi chote ambacho sisi kama Wizara ya Fedha tumekuwa tukitembea kwenye halmashauri mbalimbali kutoa elimu ya kifedha, moja ya ajenda pia ambayo tunaibeba ni hii bima ya kilimo.
Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba, hata maoni ya wadau na wakulima wadogo haya, nayo yamezingatiwa na kanuni hizi ambazo sasa zitaanza kutumika katika mwaka huu wa fedha 2026/2027. Ahsante.
Name
Lucy Edward Mwakyembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Kanuni za Bima za Kilimo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali?
Supplementary Question 4
MHE. LUCY EDWARD MWAKYEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza na nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali kwa ajili ya uanzishwaji wa bima hii ya kilimo.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kilimo ndiyo suluhisho la kumkomboa Mtanzania katika ajira, wakiwemo vijana, je, Serikali inaonaje kuongeza kasi ya utafiti katika kukamilisha na kutumika bima hiyo hasa kwa upande wa bima ya mazao, mvua nyingi, ukame, wadudu kwenye mimea, pamoja na dhoruba. Matukio haya yanasababisha wananchi kupata majanga ya asili ambapo bima ikianza kwa haraka walau itampunguzia maumivu mwananchi. (Makofi)
Name
Laurent Deogratius Luswetula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali zuri la nyongeza, kwanza bima hii ya kilimo, nikiri kabisa kwamba imeanza kama miaka miwili au miaka mitatu huko nyuma. Kwa maana hiyo, katika hali ya kawaida kulingana na maoni ya wadau ambayo tumeendelea kuyapokea mpaka sasa hivi, jambo hili na utafiti huu ulitakiwa uchukue muda mrefu zaidi wa miaka hii miwili au mitatu ambayo sisi kama Wizara ya Fedha tunaweza kutumia.
Mheshimiwa Spika, kwa maana hiyo, yeye ameuliza kwamba kuona namna ya kuweza kuharakisha; kwanza sisi kama Wizara ya Fedha tumeharakisha na kwa sababu hiyo, kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi, uharakishwaji huo na ndiyo maana tunaenda kutekeleza zaidi, kanuni hizi katika mwaka wa fedha 2026/2027 kuanzia Julai 1, 2026.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved