Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 43 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 516 | 2026-06-04 |
Name
Moses Charles Bujaga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sumve
Primary Question
MHE. MOSES C. BUJAGA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Malya – Nyambiti (kilometa 58) ili kuboresha usafirishaji katika Jimbo la Sumve?
Name
Abdallah Hamis Ulega
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkuranga
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moses Charles Bujaga, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Malya – Nyambiti, kilometa 58 kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kufahamika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved