Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 43 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 516 2026-06-04

Name

Moses Charles Bujaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. MOSES C. BUJAGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Malya – Nyambiti (kilometa 58) ili kuboresha usafirishaji katika Jimbo la Sumve?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moses Charles Bujaga, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Malya – Nyambiti, kilometa 58 kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kufahamika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.