Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 43 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 517 2026-06-04

Name

Salum Khamis Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. SALUM K. SALUM aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa Mradi wa Barabara ya Nkoma – Lalago kilometa 65?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salum Khamis Salum, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mkataba wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Nkoma – Lalago kilometa 65 umesainiwa kati ya Serikali na Kampuni ya ujenzi ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC). Serikali inaendelea na taratibu za malipo ya awali ili kuwezesha mkandarasi kuanza kazi za ujenzi.